MIFUMO PESA NA MAENDELEO YAKE
UTANGULIZI
Pesa ni mfumo utumikao kuwasilisha uhalali wa thamani ya kitu fulani au bidhaa ndani ya miliki , himaya au sehemu fulani.
HISTORIA YA PESA NA MIFUMO YAKE
Hadi sasa pesa imeweza kupitia mifumo mikuu mitano katika matumizi yake ya kufanya biashara ama kununulia bidhaa na mifumo hiyo ni kama ifuatavyo:-
1 Mfumo wa kubadilishana bidhaa kwa kitu(barter trade)1: MFUMO WA KUBADILISHANA BIDHAA KWA kITU
2 Mfumo wa zana za chuma(iron trade)
3 Mfumo wa karatasi(paper money)
4 Mfumo wa plastiki( credit card)
5 Mfumo wa kidigitali(cryptocurrency)
![]() |
| Biashara ya mabadilishano |
Huu ni mfumo uliokuwa mahususi hapo zamani katika kipindi cha zama za mawe za kwanza ambapo binadamu walitumia njia ya mabadilishano ya kitu kwa chakula kama nafaka , wanyama ilikuweza basi kukidhi mahitaji yao. Hivyo njia ya mabadilishano ilitumika kama mfumo wa pesa.
2: MFUMO WA ZANA ZA CHUMA
![]() |
| Zama za chuma |
Huu ni mfumo ambao binadamu walikuwa wakiutumia kupata vitu kwa mabadilishano ya chuma na bidhaa fulani. Katika kipindi cha zana za kati za mawe mfumo huu uliweza kutumiwa kwa kiasi kikubwa. Kwa lugha ya kitaalamu ulijulikana kama iron trade system. Wageni kutoka mataifa ya ulaya walikuwa wakija afrika na kufanya biashara hiyo kwa mabadilishano yaliyoelezewa hapo juu.
3: MFUMO WA KARATASI
![]() |
| Pesa za noti |
Huu umekuwa ni mfumo mama wa pesa hadi sasa ambao unatumiwa dumia nzima na kuwekwa thamani ya uhalali kwenye karatasi ama maarufu kwa jina la noti. Mfano kwa nchi za afrika mashariki ikiwemo Tanzania ambao wanatumia tsh Kenya wanatumia ksh na Uganda wanatumia pia ugsh.
4: MFUMO WA PLASTIKI
![]() |
| Kadi ya benki |
Vile vile pesa haikuweza kuishia hapo ikaja hadi kwenye mfumo wa plastiki yaani hapa inakuwa katika mfumo wa kadi ujulikanao kama credit card. Hapa mabenki ndio wahisika wakuu wa mfumo huu. Pia unasaidia kupunguza idadi ya kiasi kikubwa cha pesa kukaa katika sehemu salama na rahisi kuhifadhika.
5: MFUMO WA KIDIGITALI
Pesa ya kidigitali( Bitcoin)
Maendeleo ya teknologia na maendeleo ndio yaliyopelekea kuingia kwa pesa mpya zilizokuwa katika mfumo wa kidigitali yaani kwa lugha ya kitaalam tunaita cryptocurrency.
Mfumo huu wapesa uliweza kufanikiwa kutumika mnamo mwaka 2009 na jamaa aliyejulikana kama Satosh Nakamoto mjapani mwenye asili ya kiamerika wakati aliponunua pizza 2 kwa thamamani ya aina ya pesa aliyoitumia iliyokuwa ikijulikana kama Bitcoin ambazo kwa idadi ya thamani zake ilikuwa Bitcoin elfu kumi. Hadi sasa hakutaka kujulikana kama ni yeye mwanzilishi wa hiyo aina ya pesa kwa sababu alinukuu na kusema hiyo ni pesa ambayo inamilikiwa na watu wote wa ulimwengu huu.
Hadi sasa Bitcoin ndio pesa iliyokuwa na thamani kubwa duniani ukilinganisha na mifumo mingine ya pesa.





This is official blog for sharing ideas
ReplyDeleteGood idea...and supportive
ReplyDeleteThanks for your co operation๐๐ฟ๐๐ฟ๐๐ฟ
Delete